MLAJI
1;Enyi walaji wa
leyo, kusema nanyi nataka
Ipunguzeni
pupiyo, lasivyo mtadhurika
Nyoyo zipeni
zuiyo, mwili utabusarika
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
2;Mnapopita
shambani, matunda yawazuzuwa
Mboga hamzitamani, zawachosha
kuchambuwa
Macho yote
yamtini, paku mnaupekuwa
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
3;Muonapo tunda
pera, limelala kidarini
Nyanyachungu ama
tura, mbili mbili zi tawini
Kwa kebehi
mnafura, mwasema hizi za nini
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
4;Mwataka
ulojazia, mti hadi mashinani
Ili
ukiupandia, uhisi u kitandani
Huku dodo
wajilia, wajipea burudani
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
5;Muonapo ni
papai, au dodo mwalichuma
Mwajitia
ubedui, kulipapasa kwa nyuma
Kifuatacho
jimai, kichwani mwawaza nyama
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
6;Kisha hufata
vurugu, za kwichi kwichi mtini
Yale mavuno ya
njugu, mlizokula shambani
Leo mwazimwaga
mbegu, kwa mineso matawini
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia
7;Ladha ya tunda
nanasi, madodo ama balungi
Haipimwi kwa
nafasi, ama kujazia vingi
Maviru yana
virusi, iogopeni mitungi
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
8;Najua shida ni
moyo, walaji mwataabika
Mwashindwa weka
zuiyo, kula vilo sitirika
Mwafulani
shauriyo, mauti yatakufika
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
9;Alisema
muandishi, tamayo kuihusudu
Kwa hati ya
maandishi, madodo yana wadudu
Msitilie
ubishi, ama takufa kibudu
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
10;Tama Aisha
Johari, tembeeni na pakacha
Imechafuka
bahari, refarii kawa kocha
Msivimbishe
vidari, mtageuzwa chamcha
Shikilia wako
moyo, mlaji utaumia.
*MWISHO*
Mtunzi: Husein.R.Kaparata
TEL.0714631510
Email.huseinkapa112@gmail.com

Comments
Post a Comment