Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2022
                    MLAJI 1;Enyi walaji wa leyo, kusema nanyi nataka Ipunguzeni pupiyo, lasivyo mtadhurika Nyoyo zipeni zuiyo, mwili utabusarika Shikilia wako moyo, mlaji utaumia.   2;Mnapopita shambani, matunda yawazuzuwa Mboga hamzitamani, zawachosha kuchambuwa Macho yote yamtini, paku mnaupekuwa Shikilia wako moyo, mlaji utaumia.   3;Muonapo tunda pera, limelala kidarini Nyanyachungu ama tura, mbili mbili zi tawini Kwa kebehi mnafura, mwasema hizi za nini Shikilia wako moyo, mlaji utaumia.   4;Mwataka ulojazia, mti hadi mashinani Ili ukiupandia, uhisi u kitandani Huku dodo wajilia, wajipea burudani Shikilia wako moyo, mlaji utaumia.   5;Muonapo ni papai, au dodo mwalichuma Mwajitia ubedui, kulipapasa kwa nyuma Kifuatacho jimai, kichwani mwawaza nyama Shikilia wako moyo, mlaji utaumia.   6;Kisha hufata vurugu, za kwichi kwichi mtini Yale mavuno ya njugu, mli...
            BWANA DHIKI 1;Hana baba wala mama,wala ndugu wa kunusa Halali ndani ya hema,jua mvua yamtosa Ngozi yake ya ukoma,ngumu kwa kuipapasa Wamuita bwana dhiki,jinale yake maisha.   2;Hana kazi wala bazi,anafanya dei waka Elimu hana ujuzi,darasani hakufika Machinga na wachuuzi,humfanya kibaraka Wamuita bwana dhiki,jinale yake maisha.   3;Kuu kuu nguo zake,mabwende yalotoboka Waume kwa wanawake,husema amechizika Upitapo kando yake,uvundo unamnuka Wamuita bwana dhiki,jinale yake maisha.   4;Sura yake ni nyeusi,tii yenye kupauka Mfupi kama kipisi,ama shina la mugoka Mapele kama fenesi,ngoziye imebabuka Wamuita bwana dhiki,jinale yake maisha.   5;Watupavyo jalalani,vyote vilo haribika Ndizi mboga za majani,na nyama zinazo nuka Hushindilia tumboni,haogopi kudhurika Wamuita bwana dhiki,jinale yake maisha. 6;Yupo peku miguuni,kokoto zinamng'ata Apitapo jalalani,vigae v...
      MTWANGAJI 01:Nianze na wa nyumbani, salamu kuwatolea Jamani mu hali gani, zipoje zenu afia Nanyi wa ughaibuni, amani nawatakia Naringia mtwangio, unaniweka mjini.   02:Niwajuze yangu fani, kwa dhati nilobobea Si fundi wa cherehani, dereva na abiria Wala ticha darasani, zote sijazizoea Naringia mtwangio, unaniweka mjini.   03:Si nguvu bali akili, ndio ninayotumia Kinu ninakikabili, mtwangio kushushia Mimi fundi kwelikweli, kutwanga nimebobea Naringia mtwangio, unaniweka mjini.   04:Nikiziona nafaka, zimetulia kinuni Unanipanda wahaka, nasisimuka mwilini Mchi mate naupaka, tayari nipo kazini Naringia mtwangio, unaniweka mjini.   05:Tena kutwangia kinu, kisikalie pembeni Zisije kufeli mbinu, mchi ukatwanga chini Kina mwajuma na tunu, wanione punguani Naringia mtwangio, unaniweka mjini. 06:Ukitua mtwangio, kusaga hizo nafaka Hubakia mshangao, kinu kina taabika Nakaa kila mkao, ufaao kutwangika Naringia mtwangio, unaniweka mjini.   07:Umakini na...